Imelda Mtema/mchanganyiko
MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Cyrill Kamikaze ‘Cyrill’ na Mbongo Muvi Sabrina Omary ‘Sabby’ hivi karibuni walinaswa katika ufukwe wa Hoteli ya Golden Tulip, Masaki jijini Dar wakiwa kimahaba na hivyo kuzidisha tetesi kuwa wanatoka kimapenzi.

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Cyrill Kamikaze ‘Cyrill’ na Mbongo Muvi Sabrina Omary ‘Sabby’ wakipozi kimahaba.
Chanzo chetu makini kilisema wawili hao walionekana hotelini hapo wakiwa eneo la kuogelea na walipomaliza walihamia katika viti ambako sasa walikumbatiana kimahaba kana kwamba hakuna mtu anayewaona.
Kwa nyakati tofauti walipoulizwa kuhusu tetesi za kuwa wapenzi na ushahidi wa picha, kila mmoja alikana, wakidai zitakuwa ni picha za kutengenezwa kwa sababu mchezo huo umekuwa maarufu siku hizi huku Sabby akisisitiza kuwa angefika ofisini ili kujiridhisha na picha hizo ndipo aweze kuzungumza, kitu ambacho hakukifanya.
Hamida Hassan/mchanganyiko
UKARIBU wa mastaa wa filamu za Kibongo, Kulwa Kikumba maarufu kama Dude na msanii mwenzake Ester Kiama unaonyesha kama kuna kitu kati yao baada ya kuonekana kuwa karibu kwa muda mwingi kiasi kinachotia shaka!
Staa wa filamu za Kibongo, Kulwa Kikumba maarufu kama Dude.
Chanzo kilicho karibu na wawili hao kimesema mara kwa mara wanaonekana kuwa karibu kila wanapokwenda na kuonyesha dalili zote za kimahaba, lakini wenyewe wanadai ni washkaji walio kazini.
Gazeti hili lilibahatika kuwafuma wakiwa pamoja na walipoulizwa juu ya tuhuma za kujihusisha kimapenzi, kila mmoja alimtupia msalaba wa kujibu mwenzake.  “Mh, jibu wewe, mimi najua Dude ni kaka yangu na ni mfanyakazi mwenzangu”, alisema Ester.
KWAKO mtaalamu wa Hip Hop uliyeibeba Ilala nzima begani, Rashid Makwilo ‘Chid Benz’, mambo vipi mzazi mwenyewe? Uko poa? Mishe zinasemaje?
Ukitaka kujua hali yangu, mimi niko poa na ninaendelea na majukumu yangu ya kujenga taifa kama kawaida na barua hii ni sehemu ya majukumu yangu ya kazi hivyo lazima nikuandikie tu, sina jinsi.
Dhumuni la barua hii kwanza kabisa ni kutaka kukukumbusha kidogo umuhimu wako katika jamii. Sitaki kuamini kwamba hujui umuhimu wako lakini kukumbushana ni muhimu, binadamu tumeumbwa kusahau.
Chid wewe ni mwakilishi mzuri sana wa Muziki wa Hip Hop. Tangu kipindi kile ulichosumbua na wimbo wako wa Dar es Salam Stand Up na nyingine kibao.Ulikuwa hukosei, ulikuwa unaachia jiwe baada ya jiwe na kila mtu alikuwa anakubali uwezo wako.
Kudhihirisha wewe ni mkali, nakumbuka ulikuwa ni lulu katika suala zima la kolabo. Wasanii walikuwa wakipanga msururu kukusaka, waliamini ukiingiza sauti yako katika nyimbo zao basi nazo zitakuwa tamu kama mcharo.
Hilo halikuwa na kificho, ulifanya kolabo nyingi sana. Nyimbo kama Neila ya Tunda Man, Hao na nyingine kibao zilinoga sana pale ulipoingiza sauti yako yenye mamlaka ambayo ulijua kuipangilia na kuendana na biti, wewe ni mkali aisee!
Pamoja na uzuri huo, juzikati hapa liliingia suala la wewe kunaswa na madawa ya kulevya. Binafsi sikushtuka sababu dalili za wewe kutumia nilishaziona kabla.Niliona dalili kutokana na matendo yako, yalikuwa hayafanani na uwezo wako mkubwa wa kutunga mashairi yenye uzito. Matukio kama yale ya kumdunda msanii mwenzako, Rehema Chalamila ‘Ray C’, nilijua kabisa si wewe.
Lilipokuja kutokea lile la kukamatwa na madawa pale Air Port, nilisikitika sana kama shabiki wako. Suala la wewe kuanza kuingizwa kwenye mikono ya sheria ni kuzidi kudidimiza kipaji chako na muziki wako kwa jumla.
Nilifuatilia kwa makini kesi yako hadi pale ulipotakiwa kulipa faini nikasema ni jambo la heri lakini unapaswa sasa kubadilika kweli na kutokubali kurudi nyuma. Uliwahi kukiri kuwa unatumia madawa, ukaahidi kuacha lakini ukarudia.
Nikushauri, mimi pamoja na mashabiki wengi Bongo na nje tunakupenda na tunahitaji kuendelea kusikia ‘madini’ yako.Ngoma yako ya Kimbiza ambayo haina muda mrefu sana tangu uiachie inatosha kuonesha kwamba uwezo unao, tupe raha kama ile ambayo ulikuwa unatupa.
Achana kabisa na madawa ya kulevya, sitegemei kukuona tena unakamatwa au unahusishwa katika suala hilo kwa namna yoyote.Ni matumaini yangu utabadilika kweli, kwa leo ni hayo, kila la kheri!
Shani Ramadhani/Mchanganyiko
MWANADADA anayefanya vizuri katika muziki na filamu nchini, Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole, ameendeleza tabia yake ya kumpa vipigo vya mara kwa mara mpenzi wake, Naftar Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ ambaye pia ni msanii.
Mwanadada anayefanya vizuri katika muziki na filamu nchini, Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole akiwa na mpenzi wake Nuhu Mziwanda.
Habari kutoka vyanzo vya kuaminika vinasema Shilole alimdunda kwa mara nyingine Nuh wiki iliyopita, baada ya kutokea kutoelewana baina yao kwa kile kinachodaiwa kuwa ni wivu wa kimapenzi.
“Ninampenda sana mume wangu na ninamheshimu, hili suala linapozungumzwa au kuulizwa linaniumiza sana, haya ni mambo ya muda mrefu na yameshamalizika,” alisema msanii huyo nyota wa kibao cha Malele.
Kwa upande wake Nuh alipotafutwa, simu yake haikupatikana hewani na hata alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno na kuulizwa kuhusu jambo hilo pia hakujibu.Hii siyo mara ya kwanza kwa wapenzi hao kukwaruzana, kwani imeshawahi kutokea siku za nyuma hadi kufikia wakati wakatengana.

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget