
Wadukuzi hao ambao wanajiita Lizard Squad wameivamia tovuti hiyo ya www.malaysiaairlines.com na kuweka picha ya mjusi huyo ambaye amevaa kofia akiwa na kiko na koti maalum litumikalo kwenye milo ya jioni. Picha hiyo iliambatana na wimbo maalum wa ‘rap’.
Katika taarifa yake, shirika la Malaysia Airlines lilikiri kwamba tovuti yake imevamiwa na watumiaji wake walikuwa wakielekezwa kwenye tovuti ya wadukuzi hao.
Hata hivyo, taarifa hiyo ilieleza kuwa tatizo litakuwa limetatuliwa ndani ya saa 22.