Will Smith akiwa na familia yake.
STAA wa filamu Will Smith na mkewe Jada Pinkett wanataraji kusherehekea miaka 20 katika uhusiano wao mbali na kuwa wanandoa hao walisherehekea miaka 17 ya ndoa yao Desemba 31, mwaka jana.
Will Smith na mkewe Jada Pinkett.
Jada mwenye umri wa miaka 43, aliandika katika ukurasa wake wa Facebook kuhusu uhusiano wake na Will huku akielezea matunda ya mahusiano hayo wakiwemo watoto wao
Willow na Jaden Smith na jinsi walivyoweza kudumu katika upendo na kuvumiliana.
Aliandika hivi: Desemba 31, mwaka jana, nilisherehekea miaka 17 ya ndoa. Mwezi Februari mwaka huu nitatimiza miaka 20 tangu nilipoamua kuanza maisha na Will. Nimejifunza kuwa muungano wa watu wawili ni muujiza wa kweli na watoto ndiyo matunda ya muujiza huo.
Kwa jinsi ninavyoendelea kuupanda mlima huu wa upendo na muungano, ninahamasika kuona yote ambayo yeye na mimi tumetengeneza tukiwa kileleni mwa mlima huo. Aliandika Jada katika sehemu ya ujumbe huo.

Pichani kulia ni picha ya mjusi iliyowekwa kwenye ukurasa wa mbele wa tovuti ya Shirika la Ndege la Malaysia.
WADUKUZI wa mitandao wameweka picha ya mjusi  na wimbo katika tovuti ya Shirika la Ndege la Malaysia ambamo wameweka ujumbe  usemao kwamba ‘Ndege Haipatikani’ ukihusishwa na ndege namba MH370 ya shirika hilo ambayo ilipotea mwaka jana mwezi Machi  na haijapatikana mpaka leo.
Picha iliyowekwa kwenye tovuti hiyo ikiambatana na wimbo wa 'rap'.
Wadukuzi hao ambao wanajiita Lizard Squad wameivamia tovuti hiyo ya www.malaysiaairlines.com na kuweka picha ya mjusi huyo ambaye amevaa kofia akiwa na kiko na koti maalum litumikalo kwenye milo ya jioni. Picha hiyo iliambatana na wimbo maalum wa ‘rap’.
Katika taarifa yake, shirika la Malaysia Airlines lilikiri kwamba tovuti yake imevamiwa na watumiaji wake walikuwa wakielekezwa kwenye tovuti ya wadukuzi hao.
Hata hivyo, taarifa hiyo ilieleza kuwa tatizo litakuwa limetatuliwa ndani ya saa 22.
Rais wa 16 wa Marekani Abraham Lincoln
Vitu vya kumbukumbu vya aliyekuwa rais wa 16 wa Marekani Abraham Lincoln vimeuzwa katika mnada mjini Dallas nchini Marekani na kupata dola 800,000.
Msokoto mmoja wa nywele za rais huyo aliyeuawa umeuzwa kwa dola 25,000 lakini barua iliokiri kwamba vita vya wenyewe kwa wenyewe havikuwa vizuri haikuuzwa.
Barua iliotiwa sahihi na naibu wake John Wlkes Booth iliuzwa kwa dola 30,000 huku agizo lake la kijeshi likitia kibindoni dola 21,250.
Vitu vya Lincoln vilipigwa mnada mjini Dallas marekani
Ukusanyaji wa vitu hivyo 300 ulianzishwa mwaka 1963 na mmiliki wa jumba la sanaa Donald Dow aliyefariki miaka mitano iliopita.
Mwanawe Greg amesema kuwa ni wakati wakusanyaji wengine wapate fursa ya kuifurahia.
Amesema kuwa babaake alikuwa ameanza ukusanyaji huo kutokana na maslahi yake katika vita vya wenyewe kwa wenyewe pamoja na historia ya kijeshi,lakini baadaye alikuwa na hamu na Lincoln na mauaji yake.
Stori Na Musa Mateja/Ijumaa Wikienda
BAADA ya kukiri kwa mdomo wake kutumia madawa ya kulevya ‘unga’ na baadaye ‘kustaafu’, madawa hayohayo yamemletea msanii Rehema Chalamila ‘Ray C’ ‘msala’ ambao umemfanya yeye mwenyewe, kwa hiari yake, bila kusukumwa ajisalimishe polisi.
Msanii wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ akiwa Hospitali ya Mwananyamala .
Hivi karibuni, Ray C alijikuta akiangua kilio ndani ya Kituo cha Polisi cha Kijitonyama ‘Mabatini’, Dar baada ya kuhusishwa na ishu ya uuzaji wa unga.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, Ray C au Kiuno Bila Mfupa alidai alishtukiwa na mtu wa intelejensia (usalama wa taifa) ambaye amekuwa akimfuatilia kutoka nyumbani kwake Mbezi Beach, Dar anakoishi kwa sasa.
KAWE DARAJANI
Chanzo hicho kilinyetisha gazeti la Ijumaa Wikienda kwamba, siku ya tukio, wakati Ray C akitokea nyumbani kwake, alipofika maeneo ya Kawe Darajani aliona pikipiki ikimfukuzia na baadaye ikampita na ‘kumbloku’ kwa mbele.
Ilisemekana kwamba baada ya kusimama, jamaa alishuka kwenye pikipiki kisha akamwambia aegeshe pembeni gari lake aina ya Toyota Carina TI.
Ray C katika pozi.
Chanzo kilidai kwamba, Ray C alikataa kufanya hivyo kwa kuhisi aliyekuwa akimwamrisha ni jambazi.
Ray C alimua kuondoa gari kwa kulazimisha ambapo alimkwepa jamaa huyo kisha kukanyaga mafuta ambapo gari liliondoka kwa kasi.
LUGALO
Ilisemekana kwamba baada ya kufika kwenye kituo cha daladala cha Lugalo alisimama na jamaa huyo aliyekuwa akimfukuzia akaegesha pikipiki mbele yake na kumtaka Ray C ashuke ndani ya gari kwani alitaka kulipekua akimwambia kuwa alikuwa amebeba unga.
Ishu hiyo ilizidi kumtia Ray C wasiwasi na kumuuliza jamaa huyo ni nani ambapo alitoa kitambulisha kuwa yeye ni askari.
Kwa kuwa hakuwa na sare, Ray C hakuamini jambo lililosababisha jamaa huyo kumuonesha kitambulisho kilichokuwa kimechakaa.
‘Ray C’akiingia kwenye gari lake aina ya 'Toyota Carina'.
MAELEWANO YASHINDIKANA
Baada ya kuona hivyo, Ray C alimwambia waongozane hadi Kituo cha Polisi cha Oysterbay lakini jamaa huyo alikataa na kumtaka waende Kawe jambo ambalo Ray C alishindwa kuafikiana nalo na kuondoa gari lake akimwambia waambatane hadi kituo kidogo cha  Polisi cha Mwenge.
Jamaa huyo alionekana kutotaka kwenda hivyo Ray C aliondoa gari kwa kasi na kuelekea Mwenge ambako alikuwa akiomba msaada kwa matrafiki na alipoona wanachelewa aliondoa gari kumkimbia jamaa huyo.
Ilisemekana kwamba awali alitaka kukimbilia Kituo cha Polisi cha Mwenge lakini alipoona kuna msongamano alikimbia kwenda kujisalimisha Mabatini huku akiangua kilio.
Taarifa zilidai kwamba jamaa huyo aliendelea kumfukuzia Ray C hadi Mabatini ambapo yeye alibana nje wakati Ray C akiwa kwa mkuu wa kituo.
Hata hivyo, baadaye jamaa huyo naye alijisalimisha kwa mkuu wa kituo ambapo naye alijieleza kwamba aliambiwa na watu wa usalama kuwa afuatilie gari hilo lililohisiwa kubeba unga.
Ilielezwa kwamba mkuu huyo wa kituo ameamuru jamaa huyo kuchunguzwa ili kubaini malalamiko ya Ray C.
Mwanadada kiuno bila mfupa 'Ray C'.
BOFYA HAPA KUMSIKIA RAY C
Baada ya kushibishwa taarifa hiyo, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Ray C ambaye alielezea mkasa mzima.
Alifunguka: “Ni kweli ulivyoambiwa tulitoka Lugalo na kuelekea Mwenge baada ya kufika kwenye Makutano ya Mwenge niliwaona askari wawili na trafiki akiwa pembeni nikawasimamisha na kuwaeleza.
“Askari mmoja alikubali kupanda kwenye gari langu nikaenda naye hadi Mabatini.
“Baada ya kufika Mabatini nilieleza kila kitu kwa mkuu wa kituo hivyo akaniambia nisiwe na wasiwasi.
“Baada ya hapo mkuu wa kituo aliita askari wa kike na wa kiume nikaongozana nao hadi katika gari langu na kupekuwa kila sehemu lakini wakasema hapakuwa na chochote kibaya, hivyo nikawa nalia tu na mkuu wa kituo akaniomba ninyamaze na kuniruhusu nikaondoka zangu kwenda Mwananyamala hospitali kumeza dawa.
“Kama kweli alikuwa ni mtu wa usalama au askari, alitakiwa kuvaa sare na kufuata utaratibu wa kunipekua na siyo kunikimbiza kwani nilijua ni jambazi.
“Nusura nife kwa presha kwani nilijua ni mtu mbaya tu anataka kunidhuru afya yangu, lakini namshukuru Mungu sikupaniki zaidi ya kulia. Hata hivyo mkuu wa kituo ameahidi kulishughulikia suala hilo kwa kufanya uchunguzi baada ya jamaa huyo naye kujisalimisha polisi.”
Muigizaji Tino Madhahabu enzi…
Stori: waandishi Wetu/Ijumaa
HOFU! Waigizaji wa tasnia ya filamu Tanzania, ambao walikuwa wameanza kusahausahau misiba mfululizo iliyowatokea miaka michache iliyopita, juzikati walijikuta wakitoneshwa kidonda, baada ya kutokea kifo cha muigizaji Tino Madhahabu, kilichotokea Tunduma mkoani Mbeya, kufuatia kuugua kwa muda mrefu.
Muigizaji Tino Madhahabu enzi za uhai wake.
Msanii huyo aliyetamba katika uigizaji akiwa na Dude katika kipindi maarufu cha Bongo Dar es Salaam, kwa muda wa miaka saba na baadaye kuingia kwenye filamu alikuwa akiugua ugonjwa wa moyo, kiasi cha kumfanya arejee nyumbani kwao kwa ajili ya matibabu, ambayo hata hivyo, yameshindwa kunusuru uhai wake.
Msanii 'Dude' aliyewahi kuigiza na Tino katiaka kipindi maarafu cha Bongo Dar es Salaam.
Kifo hicho kimeibua hofu upya kwa wasanii wa Bongo Muvi, hasa ikikumbukwa kuwa mchunguji mmoja (jina tunalihifadhi) aliwahi kutabiri kuwa, wimbi hilo la vifo litaendelea tena mwaka huu kwa wasanii na watu wengine maarufu, wakiwemo wanasiasa hivyo kuwataka kumrudia Mungu.
Msanii wa filamu Bongo Jini kabula.
Wasanii kadhaa waliozungumza na Ijumaa baada ya taarifa za msiba huo walionesha hofu ya kifo waliyonayo lakini wengi wakasema Kifo cha Tino ni mipango ya Mungu hivyo kila mmoja ajiandae tu.
Msanii aliyewahi kufanya kazi kwa karibu na Tino, Kulwa Kikumba ‘Dude’ alisema: “ Dah! Ni kweli jamaa katutoka, kikubwa tumuombee na hilo la hofu ni vyema kila mmoja akawa nayo ili aweze kujiandaa kwa safari.”
Msanii wa filamu Bongo, Devota Mbaga.
Katika kuonesha kuweweseka, msanii mwingine wa filamu, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ alisema: “Mimi sitakufa kwa kuwa niko karibu na Mungu, watakaokufa ni wale walio mbali na Mungu.”
Msanii mwingine, Isabela alisema kifo cha Tino kimemshtua mno na kusema ni mapenzi ya Mungu, lakini akaponda utabiri wa mchungaji akisema hajawahi kuamini mambo hayo, kauli ambayo pia ilitolewa na Rose Ndauka.
Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, kulikuwa hakuna taarifa rasmi zilizotolewa juu ya mazishi ya msanii huyo.Mungu Ilaze roho ya Marehemu mahali pema peponi. Amina- Mhariri
Imeandikwa na Hamida Hassan, Gladness Mallya na Deogratius Mongela.
Msanii huyo aliwahi kuhojiwa na Global TV Online akizungumzia ugonjwa wake pamoja na kuomba msaada hivyo ukitaka kuyasikia, fungua mtandao wa www.globaltvtz.com
 

Akiwa na umri wa miaka 90 mwanamke wa Kenya ambaye anahudhuria masomo akiwa na wajukuu zake wapatao sita inaaminika ndiye mwanafunzi mzee zaidi anayesoma shule ya msingi duniani.
Akiwa ameketi dawati la mbele kabisa darasani ,yuko darasa la tano na amevalia nguo za shule , Priscilla Gogo Sitienei anamsikiliza mwalimu anayefundisha kwa makini hukua akiandika majina ya wanyama kwa kiingereza kwenye daftari lake.
Prissilla alijiunga na shule hii ya 'Leaders Vision Preparatory School' miaka mitano iliyopita lakini pia aliwahi kuwahudumia wakaazi wa kijiji chake cha Ndalat kilichoko kwenye bonde la ufa kama mkunga miaka sitini na mitano iliyopita.
Darasani Priscilla anawasaidia wengine wafanye vyema ambao wana umri kati ya miaka 10 hadi 14 na mar azote huwaambia ujumbe wake hasa mabinti kuwa elimu ndiyo urithi wao.
Priscilla anajulikana kama Gogo maana yake bibi katika lugha ya jamii ya wakalenjini,anasefurahia masomo akiwa na umri wa miaka 90 katika umri huo anajua kuandika na kusoma pia fursa aliyoikosa alipokuwa mdogo.
Lugha ambayo Priscilla anajiona yuko huru kuitumia ni lugha mama kwake ki Kalenjin kuliko kiingereza,pindi anapotakiwa kujieleza kwanini aliamua kujiunga na shule katika umri wake.
Sababu kubwa ambayo amekuwa akiitoa,ni ajue kusoma ili amudu kusoma bibilia,lakini pia kwa umri wake anataka awahamasishe watoto kupata elimu,kwani anawaona watoto wengi wakiwa hawako shuleni na watoto hao wana watoto.
Gogo apitapo mitaani haoni shida kukabiliana na watoto ambao hawako shuleni katika muda wa masomo na kuwauliza kwanini hawako shuleni.
Gogo anasema watoto hao humjibu kwamba hawaendi shule kwakuwa umri wao ni mkubwa,name huwaambia mimi ni mkubwa sana kwenu lakini niko shuleni hivyo nanyi jiungeni na shule.
Kikubwa kinachomuumiza Gogo ni kuwaona watoto wengi waliopoteza muelekeo,wengi wao hawana baba na wanazurura hovyo mitaani,bila msaada wowote.kutokana na hali hiyo nataka kuwahamsisha waende shuleni.


Na Hamida Hassan/Ijumaa
Umbile la mwanadada aliyefahamika kwa jina moja la Avril kutoka Kenya ambaye aliwahi kudaiwa kutoka kimapenzi na Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’, hivi karibuni lilionesha kumchengua msanii wa Bongo Fleva, Omari Faraji ‘Ommy Dimpoz’ baada ya kutupia picha inayomuonesha akikitolea macho kiwowowo cha demu huyo.
Msanii wa Bongo Fleva, Omari Faraji ‘Ommy Dimpoz’ akiwa na Mwanadada Avril kutoka Kenya.
Ommy alifanya hivyo kupitia ukurasa wake wa Instragram baada kuiweka picha hiyo kisha kuanza kukisifia kijungu cha Avril kiasi cha kumfanya mmoja wa mashabiki wake atupie maoni akisema: “Unaonekana kaka wewe ni mgonjwa wa wanawake waliofungashia, ila huyu demu mkali.”
‘Ommy Dimpoz’ akitupia jicho kijungu cha Avril.
Mbali na maoni hayo mengine yaliendelea kukichambua kiumbile kizuri alichonacho mwanadada huyo na Ommy alipopigiwa simu ili kuulizwa kilichomvutia kwa demu huyo na kama anataka kujiweka kwake alikuwa akikata.



Stori:  richard Bukos na Issa Mnally/Ijumaa
Hii ni tuhuma nzito! Katika hali inayoonesha maadili Bongo yanagaragazwa kwa kiwango cha kutisha, mapema wiki hii jamaa mmoja mfanyabiashara mwenye asili ya Kihindi almaarufu Kanjibai au Ponjoro, alinaswa kitandani akiwa mtupu na mwanamke aitwaye Hidaya ambaye ni mke wa mtu, akidaiwa kudai rushwa ya ngono ili ampe ajira.
Kanjibai akiwa mpole baada ya kufumaniwa.
OFM YATONYWA
Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers, ikiwa kwenye ‘mingo’ zake ilipewa ‘ubuyu’ na vyanzo vyake kwamba ifike katika nyumba moja iliyopo Tandale jijini Dar es Salaam kwani kulikuwa na zoezi la ufichuaji wa maovu.
MAOMBI YA KAZI
Kabla ya tukio hilo, ilidaiwa kwamba hivi karibuni Kanjibai na Hidaya walikutana maeneo ya Kariakoo jijini Dar ambapo mwanamke huyo alikwenda kutafuta kazi.
Ilidaiwa kuwa baada ya kusalimiana mazungumzo mengine yaliendelea huku jamaa huyo akitaka mambo matamu-matamu ya chumbani kwa ahadi ya ajira:
“Kazi kwishapata lakini lete ile kachori (rushwa ya ngono), mimi patia kazi wewe, sawasawa?”

...Akiomba kuachiwa baada ya fumaniza hilo.
KANJIBAI ATUMA VIMESEJI VITAMU
Ilidaiwa kwamba baada ya wawili hao kuagana, Kanjibai alianza kumchombeza Hidaya kwa ‘vijimeseji’ vitamu-vitamu kupitia mitandao ya simu za mkononi hasa hizi za kisasa za kuteleza ‘smart phones’.
Iliendelea kudaiwa kwamba siku ya siku, wakiwa nyumbani kwao maeneo hayo ya Tandale, Dar, mume wa Hidaya aligundua mchezo huo mchafu baada ya kunasa mawasiliano haramu kati ya Kanjibai na mkewe ambapo alianza kumbana ‘maiwaifu’ wake ampe ushirikiano wamshike ugoni.
UTETEZI
Ilidaiwa kwamba, katika utetezi wake, mwanamke huyo alimwambia mumewe kuwa jamaa huyo alikuwa akitaka mapenzi ili ampatie ajira kwenye kampuni moja iliyopo Kariakoo, Dar.
MTEGO WAANDALIWA
Baada ya kukubaliana, mume na mke waliandaa mtego ambapo Hidaya alimwelekeza Kanjibai anakoishi Tandale.Ilielezwa kwamba, Kanjibai, bila kujua kinachoendelea huku akiomba maelekezo katika kila hatua, alifanikiwa kufika kwa wanandoa hao na kuzama ndani.Ikasemekana kwamba, jamaa huyo alipotimba ndani alikaribishwa chumbani ambapo hakuchukua muda, akasaula nguo zote na kubaki mtupu akiwa tayari kutekeleza uzinzi.

BONGE LA FUMANIZI
Baada ya Hidaya kutoa ishara kwa mumewe kuwa mambo ‘yameiva’, OFM wakatonywa ambapo bila kuchelewa, kama kawaida yake, mkuu wa zamu aliwaagiza vijana wake ambao walitoka mkuku kwa kutumia pikipiki ziendazo kasi kuelekea eneo la tukio.
OFM ilipofika eneo la tukio ilikuta bonge la sekeseke la fumanizi likiendelea huku Kanjibai akiwa mtupu kitandani, chumbani kwa wanandoa hao akiomba msamaha kwa kutumia Kiswahili cha ‘makabachori’ huku akiahidi kutorudia mchezo huo mchafu.
KISWAHILI MBOVUMBOVU
“Iko samehe mimi bana, pana jua hii kama mke ya mtu, iko najua ishi peke yake, hapana ambiya mimi kama olewa, samehe mimi ngoja ita kaka yangu jua vizuri Kiswahili ongea na wewe lakini hapana peleka mimi polisi, iko ogopa sana pelekwa Segerea,” alisikika Kanjibai akijitetea huku akimuomba mume wa mwanamke huyo pamoja na ndugu zake wamsamehe na wasimpeleke polisi kwani anaogopa kupelekwa Gereza la Segerea jijini Dar.
MKONO WA SHERIA
Hadi OFM inaanua virago eneo la tukio, mume, mke na wapambe walikuwa katika taratibu za kufuata hatua zinazostahili ili kumfikisha Kanjibai kwenye mkono wa sheria.
ONYO
Ijumaa linatoa onyo kwa vitendo viovu vya ngono na kushauri wote wanaohitaji wenza kufuata taratibu zinazostahili ili kupunguza kasi ya mafumanizi, maradhi na migogoro mbalimbali katika jamii la sivyo OFM ipo kazini kila sehemu, kila saa kuwaumbua. - Mhariri.
Na Musa Mateja/Amani
NYUMA ya ukaribu wa Rais wa Wasafi Classic Baby (WCB), Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete ‘JK’, kuna siri nzito kufuatia mambo mbalimbali yanayojitokeza kati yao kila kukicha, Amani lina cha kukujuza.
Rais wa Wasafi Classic Baby (WCB), Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete ‘JK’.
Katika kuunga maelezo hayo, inasemekana kwamba mbali na mambo mengine, hivi karibuni Diamond alimpelekea JK tuzo zake tano za kimataifa alizotwaa mwaka 2014 kwa kuwa nyuma yake kulikuwa na sapoti kubwa ya mkuu huyo wa nchi.
UKARIBU MKUBWA
Kwa mujibu wa chanzo cha karibu ambacho ni ‘mtu’ wa Diamond, staa huyo amekuwa ‘klozdi’ sana na JK kufuatia mambo yake mengi ya msingi kuyafanya kwa kumshirikisha, kiasi kwamba kuna wakati Diamond hata akikurupuka usiku wa manane kama ana jambo huwa hasiti kumpigia simu mheshimiwa na kuongea kwa muda huku wakicheka weee!
IKULU
Habari hizo zilidai kwamba hata kama Diamond akishindwa kuzungumza naye kwa simu, kukicha mguu na njia  hadi ikulu na kuzama ndani kama nyumbani kwao vile ambapo JK akiambiwa anasema ‘mwacheni aingie kijana wangu atakuwa na shida huyo’.
  ‘Diamond Platnumz’ akibadilishana mawazo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete ‘JK’.
“Diamond amekuwa na uhusiano wa karibu kwa kila jambo na JK kiasi kwamba hata yeye anamkubali vilivyo hivyo huwa hasiti kumsapoti pale anapokuwa amekwama na hata kujivunia ukaribu wake na Diamond kutokana na uchapakazi na nidhamu anayoionesha kwake kadiri siku zinavyozidi kwenda.
“Huwezi ukaongea ishu ya muziki na JK asimtaje ‘mwanaye’ Diamond, ukaribu wao umepitiliza na inasemekana wana mikakati mikubwa ya baadaye, ni siri nzito kwa kweli iliyopo baina yao na hakuna anayejua,” kilisema chanzo hicho kwa sharti la kutotajwa gazetini.
SIFA KIBAO
Akizungumza na Amani kuhusu ishu hiyo, Diamond alimmwagia sifa za kutosha  JK huku akithubutu kuanika kwamba, haoni tena katika maisha yake kama atakuja kutokea kiongozi wa juu wa nchi akawa na upendo wa hali ya juu kwa wasanii wa Tanzania kama ilivyo kwa JK.
  Tuzo ambazo Mkali ‘Diamond Platnumz’ alizifikisha kwa Rais Jakaya Kikwete.
“Kiukweli nampenda sana mheshimiwa (JK) na nimekuwa nikijiuliza kila kukicha kama kweli nchi hii tutakuja kupata rais mwenye mapenzi ya dhati na wasanii kama ilivyo sasa kwa baba yetu JK, maana ni mtu wa pekee sana kiasi kwamba muda wowote kama una shida naye yuko wazi kuzungumza na kukupanua mawazo tofauti na unavyoweza kufikiria.
KAMA MWANAFAMILIA
“Mara nyingi siku hizi ninapokutana na rais wetu nimekuwa nikijisikia kama mwanafamilia kutokana na jinsi anavyoniongoza na kuthamini kila kazi inayotokana na muziki wangu jambo ambalo ni la kujivunia sana kwenye maisha yangu maana ninaona wasanii kibao katika nchi nyingine hawafanyiwi haya tunayopata sisi wasanii wa Tanzania kutoka kwa mheshimiwa.
“Nina uhuru mwingi sana wa kuzungumza naye na amekuwa akifanya hivyo karibia kwa kila msanii na kutambua hilo na ndiyo maana hata tuzo zangu nilizopata mwaka 2014 nilimjulisha pamoja na yeye kujua na kunipongeza lakini pia mafanikio hayo naamini yamepatikana kutokana na sapoti yake kubwa ambayo amekuwa akinipatia mara kwa mara.
  ‘Diamond Platnumz’ akiwa katika pozi tofauti na rais wa nchi.
“Sidhani kama kweli tutakuja kupata rais wa aina hii ambaye amekuwa akitambua kila shughuli na fani ya kila Mtanzania maana amekuwa akitujali sana wasanii jambo ambalo halikuwahi kutokea hapo nyuma kwa marais waliopita, husasan kwenye muziki wetu huu wa Bongo Fleva,” alisema Diamond.
MARA YA MWISHO KUKUTANA
Desemba 23, mwaka jana, Diamond alikutana na JK, ikulu ambapo mbali na kumpongeza, walizungumza mambo mengi ikiwemo namna ya kujipanga zaidi kimataifa huku akimweleza madhara ya umaarufu unaendana na kupata mkwanja mrefu.
KUMBUKUMBU ZA HARAKA
Ndani ya makabrasha ya Amani, kumbukumbu zinaonesha kuwa, Diamond ameshakutana na JK si chini ya mara kumi, nje ya nchi na ndani.
Na Gladness Mallya/Amani
MSANII wa filamu Bongo, William Mtitu ameelezea jinsi alivyoteseka usiku kucha kisha kukimbizwa hospitali na kulazwa kwa saa kadhaa baada ya kuzidiwa.
Msanii wa filamu Bongo, William Mtitu akiwa hoi hospitali.
Akizungumza na Amani, Mtitu alisema kuwa hali hiyo ilitokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa malaria usiku wa kuamkia Jumanne ndipo alipelekwa katika hospitali moja iliyopo maeneo ya Magomeni Kagera, Dar alikolazwa.
“Yaani hali yangu ilikuwa mbaya, usiku sikulala kabisa nimejua kweli malaria ni hatari lakini kwa sasa naendelea vizuri baada ya kuwekewa dripu, namshukuru Mungu,” alisema Mtitu.Msanii huyo aliongeza kuwa, anaamini hali yake ilikuwa mbaya kwa kuwa ni nadra sana kusumbuliwa na malaria.
NGANA NASI KATIKA FACEBOOKTWITTER , INSTAGRAM YOUTUBE
Mikel Ruffinelli ndiye mwanamke anayejulikana rasmi kuwa na ‘mahips’ makubwa zaidi duniani.
MIKEL RUFFINELLI ndiye mwanamke mwenye ‘mahips’ (nyonga au makalio) makubwa zaidi duniani hivi sasa na ameingia katika Kitabu cha Kumbukumbu za Dunia cha Guinness.  
Mikel Ruffinelli akiwa katika pozi.
Mama huyo ambaye ni Mmarekani, anasema anajisikia raha mustarehe na umbo lake hilo alilo nalo.
Ruffinelli ambaye ni mama wa watoto wanne, mkazi wa Jimbo la California, Marekani, anasema anaishi maisha ya kawaida na kuendesha kazi zake vizuri ambapo mumewe, Reggie Brooks, pia humsifia kwamba anampenda jinsi alivyoumbika.
Akiwa amepozi na mumewe, Reggie Brooks.
Kwa mujibu wa gazeti la ‘WorldWide Werid News’, Ruffinelli alikuwa na umbo la kawaida kabisa wakati wa ujana na hakuwa na tatizo lolote la kuongezeka uzito, lakini, akiwa na umri wa miaka 22, alianza kuona ‘mahips’ yake yanazidi kuongezeka baada ya kuzaa mtoto wake wa kwanza.
Aliongeza kusema kwamba kila alipokuwa anazaa, sehemu yake hiyo ya mwili ilizidi kuongezeka mpaka akawa anashindwa kupita kwenye mlango wa kawaida.  Japokuwa kiuno chake kina inchi 40 (sentimita 102), nyonga zake zinafikia inchi 100 (sentimita 254), hali inayomfanya avunje rekodi ya dunia.
Pamoja na kwamba watu humshangaa kila anapopita na humwomba kupiga naye picha za kawaida na za video kutokana na umbo lake hilo, bado hujisikia mwenye furaha.
Anasema: “Ninapotembea mitaani, watu hunipiga picha za kawaida na za video kutoka kwenye simu zao.  Watu wengine hufikiri kwamba nilifanyiwa upasuaji ili kuupa mwonekano wa kupendeza mwili wangu, lakini ukweli ni kwamba umbo hili ni la asili.”
Ruffinelli hana mpango wa kupunguza unene wake, lakini anakiri kwamba umbo lake hilo humfanya  nyakati fulani akate tiketi  za viti viwili anaposafiri kwenye ndege, kwani kiti kimoja hakimtoshi.
Umbo lake humlazimu kupita kiubavu katika milango mbalimbali na huwa hawezi kufunga mlango wa bafu lake wakati akioga kwani sehemu ya mwili wake huwa imejitokeza nje.
Na Mwandishi Wetu/Amani
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliyeondolewa ofisini hivi karibuni kutokana na sakata la Tegeta Escrow, Anna Tibaijuka, hivi karibuni amenaswa akiwatembelea watu wanaosadikiwa kuwa wapiga kura wake jimboni Muleba mkoani Bukoba akiwa pekupeku.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof.Anna Tibaijuka akipekua jimboni Muleba mkoani Bukoba.
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali, vikiwemo mitandao ya kijamii, Waziri huyo Profesa, ameamua kuwafuata wapiga kura wake popote walipo jimboni kwake, kwa ajili ya kujiweka sawa wakati huu nchi ikijiandaa kwa Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani, Oktoba mwaka huu.
Prof.Anna Tibaijuka akiwa na watu wanaodaiwa kuwa ni wapiga kura wakejimboni hapo.
“Lile sakata la Escrow limemchanganya sana Profesa, anaamini maadui zake kisiasa wanalitumia kama fimbo ya kumchapa, anachofanya ni kuwapitia wapiga kura wake na kuwaeleza ukweli na kwa kadiri anavyozidi kuwafikia, wengi wanaonekana kumwelewa,” alisema mtu mmoja anayefuatilia safari za Waziri Tibaijuka, ambaye ni mmiliki wa kampuni ya VIP, inayodaiwa kuuza hisa zake za IPTL, James Rugemalila, alimuingizia kiasi cha shilingi bilioni 1.6 kwenye akaunti yake binafsi, fedha ambazo baadaye, mtumishi huyo wa umma alidai zilitolewa kwa nia njema, kwa ajili ya kuwasaidia kimasomo wasichana.
Prof.Anna Tibaijuka wakati akiwa Bungeni.
Katika picha zinazoonekana katika mitandao, Profesa Tibaijuka, ambaye aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Makazi wa Umoja wa Mataifa (INHABITAT), anaonekana akiwa na baadhi ya akina mama walitembelea kaya mbalimbali jimboni mwake. Aidha moja ya picha hizo, zinamuonyesha akiwa na familia moja nje ya kibanda chao cha bati.
Amani lilimtafuta Profesa Tibaijuka ili kuzungumzia suala hilo, lakini alipopatikana, aliomba kupigiwa baadaye kwani kwa wakati huo,alidai kuwepo kikaoni. Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, simu ya kiongozi huyo ilikuwa ikiita bila kupokelewa.
kidoti
  
Mbunifu wa mavazi na mtangazaji Bongo, Jokate Mwegelo amesababisha shosti yake, Wema Sepetu ‘Madam’ afurahi baada ya kumpelekea zawadi ya kandambili zake za Kidoti pamoja na vipodozi mbalimbali.
Jokate alisema Wema ni miongoni mwa watu ambao anawakubali kutokana na mchango mkubwa katika tasnia ya filamu Bongo, hivyo ameamua kumpelekea zawadi  ya bidhaa zake za Kidoti kuonesha heshima yake.
“Zawadi zangu niliwapa watu mbalimbali mmoja wapo akiwa ni shoga yangu wa kitambo Wema, hii inaonyesha ni jinsi gani nina mapenzi makubwa kwake,” alisema Jokate.  
 
Kwa upande wake Wema, alifurahi na kusema amependa zawadi hiyo anamuomba Mungu azidi kumfungulia milango Jokate katika bidhaa zake mbalimbali anazosa-mbaza.
Video ikiwaonyesha mateka wa Kijapan, Kenji Goto Jogo na Haruma Yukawa, walio katika nguo za rangi ya chungwa, wakiwa na Jihadi John anayedai fidia ya Dola milioni 200 ili kuwaachia mateka hao.
Waziri Mkuu wa Japana, Shinzo Abe, ambaye anategemewa kuokoa maisha ya mateka wa Kijapan.
Kenji Goto Jogo (kushoto) mwandishi wa habari wa Japan na Haruna Yukawa mwanajeshi kutoka kampuni binafsi, wote walikamatwa nchini Syria mwaka jana.
WAPIGANAJI wa Taifa la Kiislam (ISIS) wametoa picha za video ambapo linatishia kuwaua mateka wawili wa Kijapan kama hawatalipwa Dola milioni 200 (Sh. Bilioni 358) katika muda wa saa 72 zijazo.
Mateka hao ni Kenji Goto Jogo mwandisi wa habari aliyekuwa anaandika kuhusu vita vya ndani vya Syria mwaka jana, na  Haruma Yukawa mwanajeshi kutoka kampuni binafsi aliyekamatwa nchini Syria mwezi Agosti mwaka jana.
Tishio  hilo limekuja baada ya Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe, kuahidi kutoa kiasi hichohicho cha fedha  kama msaada usiokuwa wa kijeshi kwa nchi zinazopigana dhidi ya ISIS.
Video hiyo iliyosambazwa katika tovuti zinazohusiana na wapiganaji hao, ziliomwonyesha mpiganaji mwenye lafudhi ya Kiingereza ambaye anajulikana kama ‘Jihadi John’ aliyeonekana katika video za mauaji ya kuwakata vichwa mateka David Haines, Alan Henning (Waingereza), na  James Foley na Steven Sotloff (Wamarekani) hivi karibuni.

Stori: Kampala, Uganda
Oohoo! Wakati staa mkubwa wa muziki wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akichekelea kitendo cha mpenzi wake wa sasa, Zarinah Hassan ‘Zari’ au ‘The Boss Lady’ kunasa mimba yake, habari ya mjini huko Kampala, Uganda ni juu ya aliyekuwa mume wa mwanamama huyo, Ivan Ssemwanga kufunguka na kusema: “Naapa Zari hawezi kuzaa na Diamond.”
Staa mkubwa wa muziki wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na Zarinah Hassan, 'Zari'.
HABARI YA MJINI
Wikiendi iliyopita, vyombo vya habari na mitandao nchini Uganda ambako kuna makazi mengine ya Zari mbali na Afrika Kusini, kulipambwa na habari hizo baada ya mwanaume huyo aliyezaa na mwanamama huyo watoto watatu kuanika siri nzito juu ya ishu hiyo.
‘Ubuyu’ huo ulidadavua kwamba, kwanza jamaa huyo mwenye utajiri wa kutupwa alianza kwa kuelezea namna alivyoshtuka aliposikia Zari ni mjamzito.
ASHANGAA KUSIKIA ZARI MJAMZITO
Alisema kwamba alishangaa kusikia Zari ni mjamzito wakati ana umri wa karibia miaka 40 na watoto watatu ambao amekuwa akiwapuuza na kuendelea kuzurura na mpenzi wake mpya, Diamond sehemu mbalimbali ndani na nje ya Bara la Afrika.
Ivan Ssemwanga akiwa na 'Zari'
TATIZO UMRI?
Ilielezwa kwamba Ivan aliweka wazi kuwa amekuwa na hofu kwa kuwa Zari ni mwanamke ambaye umri umemtupa mkono hivyo anaweza akashindwa na ‘stresi’ za malezi ya mtoto mchanga.
Maoni ya Ivan ameyatoa baada ya Diamond kufichua kwamba Zari ni mjamzito huku akitupia vielelezo vya vipimo mitandaoni vikionesha kiumbe anayekua tumboni kwa mwanamke, jambo lililosababisha jamii kuamini kuwa ni Zari kwa kuwa wawili hao wamekuwa wakionekana kimahaba na kulala chumba kimoja kwenye hoteli mbalimbali.
Jamaa huyo alisema yeye ameshazaa na Zari watoto watatu na kwa pamoja walikubaliana kwamba Zari asilete kiumbe mwingine duniani.
NI AJABU?
Kwa mujibu wa Ivan, aligundua kwamba Zari hawezi kuwatunza vizuri watoto wake hivyo ni ajabu kuona anaongeza mwingine.
“Kwa ninavyomjua Zari, naapa hawezi kuzaa na Diamond,” alikaririwa jamaa huyo bila kufafanua kama mimba ambayo tayari Zari anayo itakwenda wapi.http://api.ning.com/files/BKB8rO763wH230bC6SV0Z9roW*ANLQaP38J5fIkWgTR71mmZHE3N1Cj3Btdf6KCudDqg1hFzW9On1-f3ugxzpvD5FhHW6KlS/oooi.jpg
Watoto wa Ivan Ssemwanga na 'Zari'.
UMRI WA MWISHO KUZAA NI UPI?
Kutokana na maelezo ya Ivan, Ijumaa Wikienda liliingia mzigo kutaka kujua umri wa mwisho wa mwanamke kuzaa ni upi?
Kwa mujibu wa mtaalamu wetu, umri wa miaka 41 bado mwanamke ana uwezo wa kushika mimba kama hana matatizo yoyote ya kiafya ambayo yanaweza kuzuia kwa namna moja au nyingine asishike mimba.
Mara nyingi muda hasa wa mwisho kabisa ni umri wa miaka 45 endapo pia mwanamke anakuwa hana tatizo la kiafya.
Hata hivyo, umri mzuri wa mwisho wa kuzaa kwa mwanamke unaoshauriwa ni miaka 40 kwani nyonga zinakuwa zimeanza kuchoka hasa kama mama atakuwa amezaa kabla.
TURUDI KWA ZARI
Kwa maelezo ya mtaalam wetu, hata kama mwanamama huyo anakaribia umri wa miaka 40 si kigezo cha kushindwa kumzalia Diamond hivyo kinachohitajika ni uangalizi wa hali ya juu.
Mwanamuziki Yemi Alade.
Marehemu baba yake Yemi.
MWIMBAJI maarufu wa kimataifa wa Nigeria, Yemi Alade, amezungumzia kwa mara ya kwanza kifo cha baba yake aliyefariki wiki iliyopita.
Msanii huyo wa kike aliyevuma kwa wimbo wa ‘Johnny’, alitoa kauli yake katika mtandao wa kijamii wa Instagram ambako aliandika: “Mungu ambariki. Mbingu imepata malaika mwenye thamani kubwa,” aliandika katika ukurasa wake wa Instagram akiambatanisha na picha ya baba yake.
Kuhusu mazishi ya mzazi wake huyo, Yemi alisema maelezo yatatolewa wakati muafaka.
“Asanteni sana kwa ujumbe wenu. Mipango ya mazishi itatolewa wakati ukifika,” aliandika staa huyo.

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget